Mkopo wetu wa wakulima unalenga wakulima wajasiriamali ambao wana uhitaji wa kifedha na wamekwama katika hatua za kilimo mfano kupalilia au kuvunia au kupukuchua au kusomba mazao kutoka shambani. Kiasi cha mkopo kinaanzia Tshs 100,000/- mpaka Tshs 1,000,000/- kutegemeana na mahitaji na ukubwa wa shamba na wingi wa mazao. Afisa mkopo atakutembelea na kufanya tathmini ya shamba kuona mazao na hatua inayoombewa fedha na kushauriana dhidi ya kiwango unachohitaji.